




Imeandikwa na IZINGO KADOKADO .
Mwili wa binadamu
unafanya mambo mengi ya kibaiolojia ambayo mara nyingi ni vigumu kuyaelewa.
Mwili una mifumo
mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo
hiyo inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote
yanayoweza kuhatarisha maisha yetu.
Yafuatayo ni mambo
yanayofanywa na mwili ambayo ni kati ya hiyo mifumo ya ulinzi wa mwili wa
binadamu.
1. KUPIGA MIAYO
(YAWNING)
Lengo kubwa la kupiga muayo ni kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi kwenye ubongo au baada ya ubongo kuchoka kufanya kazi.
Lengo kubwa la kupiga muayo ni kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi kwenye ubongo au baada ya ubongo kuchoka kufanya kazi.
Vile vile kama ukiwa
umechoka au una njaa husabababisha oxygen kupungua kwenye damu na kwenye
mapafu, hii hupelekea tatizo la kupumua, hivyo kupiga miayo husaidia kuingiza
oxygen ya ziada mwilini ili irudishe mwili katika hali yake ya kawaida.
2. KUPIGA CHAFYA
(SNEEZING)
Mara nyingi tunapiga chafya pale pua zetu zinapokua zimejaa bakteria wa magonjwa ambao hawahitajiki mwilini, Vumbi pamoja na takataka mbali mbali zilizoingia kupitia pua.
Mara nyingi tunapiga chafya pale pua zetu zinapokua zimejaa bakteria wa magonjwa ambao hawahitajiki mwilini, Vumbi pamoja na takataka mbali mbali zilizoingia kupitia pua.
Hivyo kupiga chafya
ni kitenda cha mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo matakataka nje yaliyoingia
mwilini.
3. KUJINYOOSHA
(STRETCHING)
Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho cha hiari ambacho lengo lake ni kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi mbalimbali za kutumia nguvu utakazokabiliana nazo kwa siku nzima. Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli ya mwili mazoezi na kuiweka sawa vilevile kunarudisha mzunguko wa damu katika hali yake ya kawaida na kumtoa mtu katika uchovu.
Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho cha hiari ambacho lengo lake ni kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi mbalimbali za kutumia nguvu utakazokabiliana nazo kwa siku nzima. Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli ya mwili mazoezi na kuiweka sawa vilevile kunarudisha mzunguko wa damu katika hali yake ya kawaida na kumtoa mtu katika uchovu.
4. KWIKWI (HICCUPING)
Najua umewahi kupata kwikwi, na mara nyingi mara baada ya kumaliza kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza ile sauti ya ajabu ya kwikwi inasababishwa na nini au kwa sabababu gani watu hushikwa na kwikwi?
Najua umewahi kupata kwikwi, na mara nyingi mara baada ya kumaliza kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza ile sauti ya ajabu ya kwikwi inasababishwa na nini au kwa sabababu gani watu hushikwa na kwikwi?
Hiyo yote
husababishwa na DIAPHRAGM (tamka DAYA - FRAM) kiungo kinachopatikana ndani ya
mwili wa binadamu chini kabisa ya kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi kubwa ya
diaphragm ni kusaidia katika upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale unapoingiza
hewa ndani (inhale) diaphragm hushuka chini ili kusaidia kuivuta hewa ifike
kwenye mapafu. Na unapotoa hewa nje (exhale) diaphragm hutulia kwa kubakia
sehem yake ili kuwezesha hewa chafu kutoka nje kupitia pua na mdomo.
Sasa basi, kuna
wakati diaphragm kubugudhiwa na kuisababisha kushuka chini kwa kasi sana jambo
linalosababisha wewe kuvuta hewa (inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida kupitia
koromeo la sauti, hewa ikifika kwenye box la sauti (larynx), sehem hiyo
hujifunga kwa haraka sana ili kuzuia hewa isipite huko na ndipo KWIKWI hutokea.
Mambo mengine
yanayoweza kuibugudhi diaphragm na kuisababisha kufanya kazi vibaya mpaka
kupelekea kwikwi ni kitendo cha kula haraka haraka au kuvimbewaITAENDELEA
Post a Comment